Huyu ndiye mchungaji aliyetangaza nia ya kugombea Urais mwaka huu kama mgombea binafsi.....



Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Stephano Moshi (SMUCCO), Mchungaji Godfrey Malisa, ametangaza nia ya kugombea urais Oktoba mwaka huu kwa tikeki ya mgombea binafsi.


Mchungaji Malisa, alitangaza azma hiyo huku Serikali ikiwa bado haijaweka bayana kuwepo kwa mgombea binafsi kwa sababu Katiba Inayopendekezwa haijapitishwa.
Mwaka 2010, Malisa aligombea ubunge Jimbo la Moshi kwa tiketi ya
Chama cha Tanzania Labour (TLP).

Alisema ameamua kuchukua uamuzi huo ili kurejesha heshim Julius Nyerere.a ya taifa, kama ilivyokuwa imejengwa na na Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu.
Hata hivyo, alisema enzi za Mwalimu Nyerere lilikuwa na heshima kubwa ndani na nje ya nchi ambapo tangu kuondoka madarakani hajaweza kupatikana kiongozi wa kuvaa viatu vyake.

“Mimi nimeishi Marekani na China…taifa letu lilikuwa linaheshimika, leo hii hata amani imeanza kutoweka kutokana na maujai ya watu wenye ulemavu wa ngozi, ujambazi na wizi wa fedha za umma,” alisema.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top