Man United yaichapa West Brom 3 ligi kuu ya Uingereza

KLABU ya Manchester United imewapa faraja mashabiki wake baada ya kikosi hicho cha David Moyes kuitandika mabao 3-0 West Brom.

Phil Jones aliifungia bao la kwanza United dakika ya 34 kabla ya Wayne Rooney kufunga bao lake la 13 msimu huu dakika ya 65 na Danny Welbeck aliyetokea benchi dakika ya 63 kuchukua nafasi ya Robin van Persie akafunga la tatu dakika ya 82.
Ushindi huo unaipandisha United hadi nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kutimiza pointi 48 kutokana na mechi 28.
 
Wayne Rooney akifunga bao la pili dhidi ya West Brom jioni hii.
Wayne Rooney akishangilia bao lake la pili dhidi ya West Brom jioni hii.

 Phil Jones akishangilia goli lake la kwanza leo jioni.











 Kikosi cha West Brom:
 Foster 5; Reid 6 (Sessegnon 60), McAuley 6, Olsson 6, Ridgewell 5.5; Yacob 5.5 (Morrison 40), Mulumbu 6.5; Amalfitano 6.5, Gera 7, Brunt 6 (Berahino 66); Anichebe 7.
 
Kikosi cha Manchester United:
 De Gea 7; Rafael 8 (Vidic 87), Jones 6.5, Smalling 6.5, Evra 6; Carrick 6.5, Fellaini 6; Mata 7, Rooney 7.5, Januzaj 6.5 (Kagawa 76); Van Persie 6.5 (Welbeck 63)



TUNAOMBA MAONI YAKO HAPA CHINI KUHUSU TAARIFA HII!!!

 

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top