Ridhiwani ashinda kwa kishindo uchaguzi jimbo la chalinze......


MATOKEO ya uchaguzi jimbo la chalinze yametangazwa usiku wa manane ambapo mgombea wa ccm amewabwaga wenzake kwa zaidi ya asilimia 80.
Matokeo hayo yanaonesha ya kuwa ccm wamepata kura 20812 sawa na asilimia86.54
CHADEMA  wamepata kura 2628 sawa na asilimia 10.93 wakati CUF wao wamepata kura 473
 saw na asilimia 1.97, NRA KURA 59 sawa na 0.25% AFP kura 78 sawa na 0.32%  kwa matokeo hayo msimamizi wa uchaguzi huo amemtangaza RIDHIWANI JAKAYA KIKWETE kuwa mbunge mteule wa jimbo la chalinze akisubiri kuapishwa rasmi na kuanza kuwatumikia wananchi wa jimbo lake la chalinze.
Wakati huo huo hapo jana Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salama Kikwete wakiongozana na Ridhiwani Kikwete, ambaye ni Mgombea Ubunge katika Jimbo la Chalinze Mkoa wa Pwani, wamejitokeza na kupiga kura katika kituo cha Msoga Jimboni humo.
Aidha kupitia mitandao ya kijamii  imeripotiwa kuwa kitendo cha Dk. Jakaya Kikwete kushiriki 'tendo halali la kikatiba’ limewawasababisha wananchi wengi kujitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi huo.

Usalama kwa Wananchi!
Wananchi wanaoshiriki uchaguzi huo wametakiwa kushiriki tendo halali la ‘Kikatiba’ kwa uhuru na kuondoa hofu ambayo imejengeka katika kipindi cha chaguzi kuwepo kwa vurugu zinazosababishwa na baadhi ya wafuasi wa vyama flani
Kamanda wa Polisi Mkoani humo, Ulrich Matei, ame sema kuwa ulinzi umeimarishwa katika maeneo yote ambayo wananchi wanashiriki kumchagua mwakilishi wa Ubunge ambapo katika vituo vyote vya kupiga kura Askari wa kutuliza ghasia ‘Field Forece’ wametawanywa katika barabara mbalimbali ili kuangalia suala la usalama linakuwepo na kuzuia vitendo vya kihalifu.
Aidha wamesema kutokana na kuwa Jimbo la Chalinze kuwa lina tarafa nne kila kituo Jeshi hilo, limelazimika kutoa magari ya Askari wa kutuliza ghasia ‘magari wawili’ ambapo amesema kuwa amezungukia katika vituo sita na kukuta hali ikiwa shwari.
“Nipende kuwashukuru wananchi wameonekana kuwa watulivu, zoezi linaenda kwa utulivu, hakuna sehemu imeripotiwa kutokea kwa kikwazo chochote, mimi mwenyewe ni shuhuda sijaona walinzi wa vyama wakishiriki vitendo vya kuleta vurugu hata kidogo” alisema Matei.
Amesema mawakala wanaosimamia wananchi kupiga kura hawajaonyesha hali ya kushawishi wapiga kura kuwa wampigie mgombea flani kura.
Hivi karibuni kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Pwani, ilikutana na viongozi wa vyama vyote vinavyoshiriki uchaguzi huo na kukubaliana kuwa watawahimiza wafuasi wao kuepuka kufanya vitendo vitakavyo hatarisha suala la amani katika Uchaguzi huo.
Wakati huo huo imeripotiwa na (Chadema) kupitia mitandao ya kijamii, ikiwemo JamiiForums kuwa, kuna gari ya (CCM) ambayo imekamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani humo likiwa na silaha.

Gari inayodaiwa kukamatwa na Polisi ni aina ya Land Cruiser Hard top, yenye namba T 630 BFJ ambayo inatajwa kuongozwa na mmoja wa Kiongozi wa chama hicho Wilaya ya Mfindi ‘hawakutaja jina lake’ ambapo baada mgombea wa Chadema, Mathayo Torongey, kuona hivyo alilazimika kutoa taarifa katika kituoni cha Polisi Chalinze ambapo Kamanda wa Polisi Mkoani humo, alitoa maagizo kwamba gari ya Askari wa kutuliza ghasia ‘FFU’ Pwani, iende kuitafuta gari hiyo na kuipeleka Polisi.

Imeripotiwa kuwa kuna Mapanga, Sime na Nondo ambazo zilikuwepo ndani ya gari hilo, huku ikielezwa kuwa hizo ni njama za kumdhuru mgombea wa Chadema.
CCM YAREJESHA JIMBO LA CHALINZE KWA KISHINDO!!!!!!!
MATOKEO ya uchaguzi jimbo la chalinze yametangazwa usiku wa manane ambapo mgombea wa ccm amewabwaga wenzake kwa zaidi ya asilimia 80.
Matokeo hayo yanaonesha ya kuwa ccm wamepata kura 20812 sawa na asilimia86.54
CHADEMA  wamepata kura 2628 sawa na asilimia 10.93 wakati CUF wao wamepata kura 473
 saw na asilimia 1.97, NRA KURA 59 sawa na 0.25% AFP kura 78 sawa na 0.32%  kwa matokeo hayo msimamizi wa uchaguzi huo amemtangaza RIDHIWANI JAKAYA KIKWETE kuwa mbunge mteule wa jimbo la chalinze akisubiri kuapishwa rasmi na kuanza kuwatumikia wananchi wa jimbo lake la chalinze.
Wakati huo huo hapo jana Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salama Kikwete wakiongozana na Ridhiwani Kikwete, ambaye ni Mgombea Ubunge katika Jimbo la Chalinze Mkoa wa Pwani, wamejitokeza na kupiga kura katika kituo cha Msoga Jimboni humo.
Aidha kupitia mitandao ya kijamii  imeripotiwa kuwa kitendo cha Dk. Jakaya Kikwete kushiriki 'tendo halali la kikatiba’ limewawasababisha wananchi wengi kujitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi huo.

Usalama kwa Wananchi!
Wananchi wanaoshiriki uchaguzi huo wametakiwa kushiriki tendo halali la ‘Kikatiba’ kwa uhuru na kuondoa hofu ambayo imejengeka katika kipindi cha chaguzi kuwepo kwa vurugu zinazosababishwa na baadhi ya wafuasi wa vyama flani
Kamanda wa Polisi Mkoani humo, Ulrich Matei, ame sema kuwa ulinzi umeimarishwa katika maeneo yote ambayo wananchi wanashiriki kumchagua mwakilishi wa Ubunge ambapo katika vituo vyote vya kupiga kura Askari wa kutuliza ghasia ‘Field Forece’ wametawanywa katika barabara mbalimbali ili kuangalia suala la usalama linakuwepo na kuzuia vitendo vya kihalifu.
Aidha wamesema kutokana na kuwa Jimbo la Chalinze kuwa lina tarafa nne kila kituo Jeshi hilo, limelazimika kutoa magari ya Askari wa kutuliza ghasia ‘magari wawili’ ambapo amesema kuwa amezungukia katika vituo sita na kukuta hali ikiwa shwari.
“Nipende kuwashukuru wananchi wameonekana kuwa watulivu, zoezi linaenda kwa utulivu, hakuna sehemu imeripotiwa kutokea kwa kikwazo chochote, mimi mwenyewe ni shuhuda sijaona walinzi wa vyama wakishiriki vitendo vya kuleta vurugu hata kidogo” alisema Matei.
Amesema mawakala wanaosimamia wananchi kupiga kura hawajaonyesha hali ya kushawishi wapiga kura kuwa wampigie mgombea flani kura.
Hivi karibuni kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Pwani, ilikutana na viongozi wa vyama vyote vinavyoshiriki uchaguzi huo na kukubaliana kuwa watawahimiza wafuasi wao kuepuka kufanya vitendo vitakavyo hatarisha suala la amani katika Uchaguzi huo.
Wakati huo huo imeripotiwa na (Chadema) kupitia mitandao ya kijamii, ikiwemo JamiiForums kuwa, kuna gari ya (CCM) ambayo imekamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani humo likiwa na silaha.

Gari inayodaiwa kukamatwa na Polisi ni aina ya Land Cruiser Hard top, yenye namba T 630 BFJ ambayo inatajwa kuongozwa na mmoja wa Kiongozi wa chama hicho Wilaya ya Mfindi ‘hawakutaja jina lake’ ambapo baada mgombea wa Chadema, Mathayo Torongey, kuona hivyo alilazimika kutoa taarifa katika kituoni cha Polisi Chalinze ambapo Kamanda wa Polisi Mkoani humo, alitoa maagizo kwamba gari ya Askari wa kutuliza ghasia ‘FFU’ Pwani, iende kuitafuta gari hiyo na kuipeleka Polisi.
Imeripotiwa kuwa kuna Mapanga, Sime na Nondo ambazo zilikuwepo ndani ya gari hilo, huku ikielezwa kuwa hizo ni njama za kumdhuru mgombea wa Chadema.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top