JESHI LA POLISI LIMEIMARISHA ULINZI MANISPAA YA DODOMA BAADA YA KUZUIA MAANDAMANO YA CHADEMA

Jeshi la polisi limeimarisha ulinzi katika maeneo yote ambayo yalitajwa na chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwa ndiyo watapitia wakiandamana kwenda kwenda Bungeni kuanzia saa 4 asubuhi ya leo.
Polisi wakiwa wamefunga kamba kati barabara ya mzunguko ya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani na chuo cha biashara CBE  kwaajili ya kuwazuia waandamanaji hao waliopanga kwenda Bungeni.
Polisi wapanda farasi wakiimalisha ulinzi katika viwanja vya nyerere Squere ambapo Chadema wamepanga kuanzia maandamano kuelekea bungeni.
Askali polisi wakiwafanya mawasiliano kwenye gari lao ambalo lilikuwa limepakia mbwa kwa ajili ya kuimalisha ulinzi katika viwanja vya Nyerere Dodoma kwa ajili ya kuwazuia waandamanaji wa Chadema walipanga kuandamana kwenda Bungeni.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top