Mwanafunzi wa kidato cha tano ajinyonga kwa shuka Hospitalini

Katika hali isiyotarajiwa, mwanafunzi wa Kidato cha Tano katika Shule ya Sekondari ya Wavulana Ihungo Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera, Ezra Gerald (19), amejinyonga hadi kufa kwa kutumia shuka ya hospitali, alikokuwa amelazwa kwa kile kinachoeleza alikuwa anasumbuliwa na homa ya matumbo.

Hata hivyo, ujumbe ulioachwa na marehemu huyo unaonesha alichukua uamuzi huo, kutokana na kuchukizwa na uamuzi wa daktari aliyemhudumia wa kumlaza ili atibiwe ugonjwa ambao hakuwa anaumwa.
Aidha, katika ujumbe huo imeelezwa alichukizwa na kitendo cha kupotezewa muda hospitalini wakati wenzake wakiendelea na masomo.

Tukio hilo limethibitishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Gilles Muroto aliyesema mwanafunzi huo alijinyonga Septemba 16 mwaka huu saa moja asubuhi.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top