Dr. Magufuli atangaza NEEMA kwa wafanyakazi nchini endapo watamchagua kuwa Rais

Mgombea urais kupitia chama cha mapinduzi Dr John Pombe Magufuli amewaahidi neema kwa wafanyakazi wote nchini wakiwemo walimu pamoja na wakulima kwa kuwalipa mishahara inayoendana na kazi zao huku akiwaonya kufanya kazi kwa kujituma kuliwezesha taifa kusonga mbele kwa kuwa serikali yake haitwavumilia wafanyakazi wazembe.
Mgombea huyo wa kiti cha urais kupitia CCM ameyasema hayo kwa wakazi wa namtumbo akiwa njiani kutokea Songea mkoani Rukwa kuelekea Masasi mkoani Mtwara kupitia Tunduru, Mangaka  Nanyumbu na hatimae Masasi huku akisimamishwa njiani mara kwa mara na wananchi waliotaka kumueleza kero zao ambapo pia amekagua ujenzi wa barabara unaoendelea na kuongeza kuwa serikali yake itaboresha mishahara ya wafanyakazi wote wakiwemo walimu lakini akawataka kufanya kazi kweli kweli kwa kuwa hataweza kuwavumilia wazembe.

Pia Dr Magufuli ambaye amekuwa akitumia usafiri wa barabara kwa kile anachokisema ni kujionea kero za watanzania badala ya kusimuliwa hii leo pekee ametembea kilomita zaidi ya 435 za barabara ya vumbi huku akiwaahidi watanzani kutowaangusha lakini pia akawasisitiza watanzania kumchagua rais anayeaminika lakini pia atakayedumisha ujirani mwema na nchi jirani pamoja na wahisani.



Jumatano ya September 02 Dr Magufuli anatarajiwa kuendelea na ziara yake mkoani Mtwara katika maeneo ya Newala, Tandahimba, Kitama Nanyamba Mtwara vijiji ni ziwani na baadae mtwara mjini kwenye uwanja wa mashujaa.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top