Watu 42 watiwa mbaroni kwa kutuhuma za kulipua nyumba ya Kamishna wa Polis Zanzibar

Jeshi la Polisi Zanzibar linawashikilia watu 42 wakituhumiwa kuhusika na mlipuko uliotokea juzi usiku katika nyumba ya Kamishna wa Polisi, Hamdan Omar Makame.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za makao makuu ya polisi Ziwani, Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam alisema hadi jana mchana watu 42 walikuwa ndani kwa ajili ya kuhojiwa na jeshi hilo.

Alisema uchunguzi unaendelea na bado watu wengine wanatafutwa kuhusiana na tukio hilo.

“Bado tunaendelea na uchunguzi wa jambo hili na tukishakamilisha tutatoa taarifa rasmi,” alisema Kamanda Mkadam.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top