DC abembeleza penzi la mrembo Lungi, akataliwa

Mmoja wa Wakuu wa Wilaya (DC) wa Kanda ya Ziwa ambaye pia ni kada kindakindaki wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mwenye mbwembwe (jina linawekwa kwenye mabano kwa sasa), anadaiwa kutamani penzi la mwigizaji wa sinema za Kibongo, Lungi Maulanga.

Mheshimiwa huyo alimuona Lungi kupitia kwa rafiki yake ambaye ni mbunge wa moja ya Majimbo ya Kanda ya Kati mwa nchi aliyekuwa mpenzi wa staa huyo.

Chanzo makini kililiambia ukurasa huu, bila kujali kuwa ni ‘shem’ wake DC huyo alianza kubembeleza penzi hasa kupitia mitandao ya kijamii huku akiomba iwe siri ili rafiki yake asimuone kuwa ni msaliti.

Hata hivyo, katika kuhofia jamaa huyo alitumwa na mbunge ili kumwona kama ni mwaminifu, Lungi alimkatalia lakini bado jamaa hajakata tamaa.

Kwa upande wake, Lungi alithibitisha mheshimiwa huyo kukosa usingizi juu ya penzi lake ilihali ni mume wa mtu mwenye familia na watoto wawili.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top