Angalia picha za mapokezi ya Lowassa makao makuu ya CUF leo.....

Hali hiyo imejitokeza leo asubuhi wakati mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa alipotembelea Ofisi Kuu ya CUFBunguruni, Dar es Salaam kwa mara ya kwanza.

Katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25 mwaka huu, Lowassa anawakilisha vyama vinne vinavyounda UKAWA ambavyo ni Chadema yenyewe, CUF, NCCR-Mageuzi pamoja na NLD.

Lowassa alifika kwenye ofisi za CUF saa 12.40 mchana lengo likiwa ni kuzungumza na viongozi wa chama hicho akiwa ni mwakilishi wao kupitia UKAWA.
Katika Safari hiyo walikuwepo pia wenyeviti wenza wa UKAWA -Freeman Mbowe (Chadema), James Mbatia (NCCR- Mageuzi) na Emanuel Makaidi (NLD).

Viongozi wengine ni Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif; Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Magdalena Sakaya; Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu; Naibu Katibu Mkuu Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu na wabunge wanaotoka vyama vinavyounda UKAWA.

Tofauti na ilivyotarajiwa kwamba, kujiuzulu kwa Prof. Lipumba kungesababisha mpasuko ndani ya CUF, badala yake maelfu ya wanachama wa CUF walifurika katika ofisi za chama hicho mapema leo kuanzia saa tatu asubuhi.

Hakukuwa na vikundi vya watu katika majadiliano kuashiria kujadili kuhusu kuondoka kwa Prof. Lipumba, badala yake nyimbo za kumsifu Lowassa na Ukawa zilitawala.

Baada ya Lowassa kukaribishwa na mwenyeji wake Maalim Seif, alisema, “…kwanza nawapa pole kwa Lipumba kuondoka,” kauli hiyo iliyopokelewa na maelfu ya wanachama wa CUF waliofurika katika ofisi hizo kwa kusema “Hatumtakiii…..Lipumba aende zake.”

Lowassa aliendelea “nilikuwa sijamaliza kusema. Nawapongeza kwa uvumivu wenu na umoja wenu katika kipindi hiki baada ya kuondoka Lipumba.

“Nimepata faraja sana kujiunga na Ukawa japo kumekuwa na misukosuko ndani ya UKAWA. Ni lazima tuwe wamoja, mtunze kadi zenu za kupigia kura. Mwaka huu lazima tushinde tena kwa kura asilimia 90 ili wakiiba asilimia 10 tusisikie,” amesema Lowassa.

Hata hivyo Maalim Seif amesema, “tumepata faraja kubwa sana kutembelewa na Lowassa. Hii ni kuthibitisha UKAWA bado tupo pamoja. Hakuna kurudi nyuma, mbele kwa mbele mpaka Lowassa aingie Ikulu. Zanzibar tupo tayari Maalim Seif ndiye rais. Tunasubili aapishwe.”

Kwa upande wake Duni amesema, wagombea wa UKAWA hawapo kwa nia ya kusaka madaraka peke yake kama ambavyo inaelezwa bali kuhakikisha CCM inaondoka madarakani na kila Mtanzania anapata haki sawa katika kunufaika na rasilimali za nchi yake.

“Kama mnavyojua, nilikuwa waziri serikalini. Juzi nimeamua kuachia madaraka baada ya kushauriana na viongozi wangu wa CUF ili nijiunge na Chadema kuhakikisha CCM inaondoka madarakani. Tayari nimeandika barua kwa rais ya kuachia madaraka. Na juzi tu nimetoka kumuaga rasmi,” amesema Duni huku akishangiliwa na umati.

Hata hivyo, katika mkutano huo Mbowe amewaambiwa wananchi na wafuasi wa UKAWA kuwa, “hii safari ya mabadiliko tumeipigania kwa miaka 25. Wapo waliopoteza maisha, kuachika, kufilisiwa, vilema na wenye kesi katika safari hii. Imekuwa ngumu. Akitoka kiongozi kati yetu akaona malengo yetu hayaendani nae. Huyo hatufai.

“Leo tuna wagombea waliojiunga na Chadema hivi karibuni na wanagombea urais na umakamu. Chadema hatugombei vyeo. Tupo tayari kufanya kazi na wenzetu bila kujali wamejiunga lini na chama.”

Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu kwenye mkutano huo amewatoa hofu wananchi kuhusu uvumi unaoenezwa kwenye mitandao kwamba “mgombea urais na mgombea mwenza wake ni lazima wawe wanachama kupitia vyama wanavyogombea kwa muda wa miezi mitatu.”

“Katiba zote mbili za Tanzania na Zanzibar ninazo hapa. Hakuna Katiba wala Sheria inayosema mgombea wa urais na makamo wake ni lazima watimize muda wa miezi mitatu tangu kujiunga na chama wanachokiwakilisha katika uchaguzi huu. Huu ni uzushi.”

Lissu amesema, masharti yanayotolewa na katiba hizo ni kwamba, mgombea wa urais na makamu wake ni lazima wateuliwe na chama cha siasa chenye usajili wa kudumu
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akiwapungua Wanachama na Wafuasi wa Vyama UKAWA waliofurika kwenye Makao Makuu ya CUF.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akikumbatiana na Mgombea Urais wa Zanzibar wa UKAWA kupitia Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, kabla ya kuelekea kwenye Makao Makuu Chama cha Wananchi CUF, Buguruni jijini Dar es salaam leo August 9, 2015, kulikofanyika Mkutano wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi CUF. 
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mgombea Urais wa Zanzibar wa UKAWA kupitia Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad na Wenyeviti wenza wa UKAWA, Mh. James Mbatia na Dkt. Emmanuel Makaidi wakitembelea kuelekea Makao Makuu Chama cha Wananchi CUF, Buguruni jijini Dar es salaam leo August 9, 2015, kulikofanyika Mkutano wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi CUF.
 
 
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Mgombea Mwenza wake, Dkt. Juma Haji Duni.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF na Mgombea Urais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akiwahutumbia maelfu ya wanachama na wafuasi wa Vyama vinavyounda UKAWA, nje ya jengo la Makao Makuu Chama cha Wananchi CUF, Buguruni jijini Dar es salaam leo August 9, 2015, kabla ya kufanyika Mkutano wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi CUF.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe akiwahutumbia maelfu ya wanachama na wafuasi wa Vyama vinavyounda UKAWA, nje ya jengo la Makao Makuu Chama cha Wananchi CUF, Buguruni jijini Dar es salaam leo August 9, 2015, kabla ya kufanyika Mkutano wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi CUF.
Mwenyekiti wa Chama cha NCCR - Mageuzi,Mh. James Mbatia  akiwahutumbia maelfu ya wanachama na wafuasi wa Vyama vinavyounda UKAWA, nje ya jengo la Makao Makuu Chama cha Wananchi CUF, Buguruni jijini Dar es salaam leo August 9, 2015, kabla ya kufanyika Mkutano wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi CUF.
Mgombea Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Juma Haji Duni akiwahutumbia maelfu ya wanachama na wafuasi wa Vyama vinavyounda UKAWA, nje ya jengo la Makao Makuu Chama cha Wananchi CUF, Buguruni jijini Dar es salaam leo August 9, 2015, kabla ya kufanyika Mkutano wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi CUF.
Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Tundu Lissu akiwahutumbia maelfu ya wanachama na wafuasi wa Vyama vinavyounda UKAWA, nje ya jengo la Makao Makuu Chama cha Wananchi CUF, Buguruni jijini Dar es salaam leo August 9, 2015, kabla ya kufanyika Mkutano wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi CUF.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akiwahutumbia maelfu ya wanachama na wafuasi wa Vyama vinavyounda UKAWA, nje ya jengo la Makao Makuu Chama cha Wananchi CUF, Buguruni jijini Dar es salaam leo August 9, 2015, kabla ya kufanyika Mkutano wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi CUF.
Mwenyekiti wa Chama cha NLD, Dkt. Emmanuel Makaidi akimpongeza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa mara baada ya kuhutubia.
 
 
Sehemu ya Wajumbe wa Mkutano wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi CUF.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top