Diamond platinum....huu ndio ukweli kuhusu Ukwasi wake

www.paparaziwetu.blogspot.com
Yale yaliojiri katika historia ya mfalme wa Takeu nchini Lucas Mkenda a.k.a Mr Nice yaweza kujirudia kwa nguli wa Bongo Fleva Nasib Abdul ‘Diamond’.

Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa utajiri wa Diamond unapukutika kwa kasi ya hatari huku ikibainishwa pia mali kuwa nyingi alizodai kumiliki ni ulaghai. Kupitia vyombo vya habari tofauti tofauti, Diamond amewahi kuelezwa kuwa na utajiri unaofikia bilioni moja au Zaidi huku vigezo vikitajwa kuwa ni nyumba nyingi alizonunua, miradi kibao aliyofungua na mtaa alionunua katika kitongoji cha Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Kuishi nyumba ya kupanga:
Tangu alipopata mafanikio ya kimuziki (2010-2014) Diamond amekuwa akiishi numba ya kupanga baada ya kuihama nyumba ya bibi yake iliyoko Tandale (katikati ya kituo cha Shule na Tanesco.) baada ya hapo alihamia mitaa ya Sinza Madukani upande wa kulia kama unatoka Shekilango kuelekea Mwenge.

Nyota ilivyozidi kung’ara alihama Sinza Madukani na kuhamia Sinza Mori jirani na baa ya Meeda upande wa kulia kama unatoka kituo cha Mori kuelekea Mlimani City. Nyumba hizi mbili hakuwa amepanga nyumba nzima, bali alikuwa akiishi upande na familia yake huku wakishea geti na wapangaji wengine.

Mwaka jana ndipo alipohamia katika nyumba nyingine iliyopo Sinza Mori jirani na Hotel ya Wanyama ambapo anaishi mpaka sasa. Swali linakuja kwamba kwa mtu anayemiliki bilioni moja au nusu bilioni anawezaje kuishi nyumba kamili isiyokuwa yake?

Nyumba nyingine inayodaiwa Kumilikiwa na Diamond ni aliyonunua Mwananyamala ambapo kwa mujibu wa watu wanaoifahamu wameeleza kuwa inahitaji marekebisho makubwa ili iweze kuitwa nyumba ya mtu mwenye utajiri wa bilioni moja. Taarifa kutoka mitaa yote ya Mwananyamala na Kinondoni, hakuna mtaa ulionunuliwa na Diamond.

Kuazima magari
Hivi karibuni Diamond amewahi kukiri kupewa gari na mfanyabiashara maarufu Mohamedi Kiumbe ‘Chief Kiumbe’.Uchunguzi wa swahilitz umebaini kuwa gari hilo hakupewa kama alivyoeleza bali aliazima kwa gia ya kutaka kulinunua, baadhi ya rafiki zake wanasema kwamba alitaka kutumia matangazo ya vyombo vya habari kuhusu kupewa gari hilo ili iwe rahisi Chief Kiumbe kuingia mkenge ameoewa gari hilo na kaka yake Chief Kiumbe. Gari hilo linalokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi milioni 200 kitu ambacho hata chizi hawezi kulitoa bure.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top