Jayz na mwanae wasusa kwenda kwenye sherehe ya harusi ya Solange



Mwanadada Solange ambaye aliamua kuachana na maisha ya usela na kuridhia ndoa naAlan Ferguson anaingia kwenye headline nyingine kuhusiana na kilichojiri kwenye party ya kuagwa iliyofanyika jana Novemba 15, Marekani.

Beyonce alitokea kwenye party hiyo ya nguvu iliyofanyika Indywood Cinema Theatre, lakini Jay Z na mwanaye Blue Ivy hawakuhudhuria, japo Beyonce alionyesha mwenye furaha na tabasamu wakati wote mbali na familia yake kutoshiriki naye.
Hivi ndivyo Beyonce alivyowasili kisela kwenye sherehe ya mdogo wake.
Hivi ndivyo Beyonce alivyowasili ‘kisela’ kwenye sherehe ya kumuaga mdogo wake.

Haijafahamika sababu ya Jay Z kutoshiriki katika sherehe hiyo, japo comments za watu wengi mitandaoni wanahisi ni ‘beef’ iliyokuwepo baina ya Jay na Solange lakini wao walishawahi kunukuliwa mara kadhaa na vyombo vya habari kwamba hakuna tofauti zozote baina yao.
“…. Mwisho wa siku familia huwa na matatizo na sisi hatuna tofauti na hiyo.. Tunapendana na katika yote sisi ni familia. Tumesahau kila kitu na tunaamini kila mmoja atafanya hivyo..”– Solange

Solange ana miaka 28 wakati Alan ana miaka 51, moja ya nukuu maarufu ambazo Solange amezisimamia ni ile inayopingana na masuala ya umri kwenye mahusiano ya kimapenzi; “…Age is an issue of mind over matter. If you don’t mind, it doesn’t matter..”

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top