Lowassa aongoza wakazi wa Mwanza kumwaga kada wa CHADEMA marehemu Alphonce

Aliyekuwa Mgombea Urais wa CHADEMA na kupeperusha bendera ya UKAWA, Mhe. Edward Lowassa akitoa salamu zake za mwisho kwa aliyekuwa M/kiti CHADEMA moa wa Geita Alphonce Mawazo aliyeuwawa kikatili kwa kukatwakatwa mapanga na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa CCM huko Busanda Mkoani Geita.

Tendo hili lilifanyika muda mfupi uliopita katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza baada ya mapema leo asubuhi mwili kutoka Bugando hospital na kuelekea nyumbani kwa baba yake mdogo ( Mchungaji Charles Lugiko) Nyegezi jijini Mwanza na kupelekwa katika viwanja vya Furahisha ambapo ibada nzima na salamu za mwisho kitaifa zilifanyika mahali hapo.
Mwenyekiti CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe akitoa salamu za mwisho kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Geita kamanda Alphonce Mawazo ambaye ameagwa kitaifa katika Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza

Mawazo aliuwawa tarehe 14/11/2015 kikatili kwa kukatwakatwa mapanga na wafuasi wa CCM huko Busanda Mkoani Geita akitekeleza majukumu yake ya Chama.
Familia ya Marehemu Alphonce Mawazo wakiendeshwa na mchungaji kwa ibaa fupi iliyofanyika nyumbani kwa baba Mdogo wa Marehemu.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top