Mteule wa
kuwania urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi katika Uchaguzi Mkuu
ujao, John Pombe Magufuli na Katibu Mwenezi wa CCM, Nape NNauye wakipiga
ngoma.
WAKATI
mteule wa Chama Cha Mapinduzi katika Uchaguzi Mkuu ujao, John Pombe
Magufuli akifahamika kama mtu makini kwenye utekelezaji wa majukumu
yake, imethibitika kuwa waziri huyo wa Ujenzi pia ni mkali kwenye
upigaji wa tumba, Risasi Jumamosi linakupa zaidi.
Mathalan,
katika uzinduzi wa daraja la Mbutu, wilayani Nzega mkoa wa Tabora,
uliofanyika Januari 7, 2013, Magufuli alionekana akipiga Tumba wakati
bendi kongwe ya Msondo Ngoma ikitoa burudani katika hafla hiyo, akiwa
sambamba na wanamuziki wa kundi hilo, Shaaban Dede na Hassan Moshi ‘TX
Jr.
Aidha,
wabunge wawili wa upinzani, John Mnyika (Ubungo) na Halima Mdee wa Kawe,
watakuwa ni mashuhuda wa uhodari wa Magufuli, kwani katika hafla ya
uzinduzi wa barabara ya Msewe- Baruti iliyofanyika miezi michache
iliyopita, mteuliwa huyo wa CCM aliifanya tena shughuli hiyo mbele ya
umati wa wananchi waliohudhuria.
Post a Comment