Kijana apoteza maisha baada ya kujeruhiwa na Kiboko........Soma zaidi hapa

 Mkazi mmoja wa kijiji cha Malili kata ya Malili Wilayani Busenda mkoani Simiyu Japhet Nhandi(18) amefariki dunia baada ya kujeruhiwa vibaya na kiboko.

Tukio hilo limetokea jana wilayani humo baada ya wananchi kupambana na mnyama huyo,kitu kilichopelekea kumuua kijana huyo.  Kaka wa marehemu aliyekuwepo katika tukio hilo John Nhandi, ameiambia Blog hii kuwa tukio hili limetokea saa 10 jioni kijijini humo wakati wa mapambano na mnyama huyo. 

Amesema baada ya kujeruhiwa vibaya walifanya utaratibu wa kumpeleka mdogo wake katika hospital ya rufaa ya bugando iliyopo jijini Mwanza,lakini wakati wakiwa njiani alifariki dunia kutokana na kujeruhiwa sana na mnyama huyo. 

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Busenda Kitusi Kamani (CCM),ambaye amehudhuria mazishi hayo kama sehemu ya mshikamano na kuwapa pole wafiwa, amesema wanachi wilayani humo wanatakiwa kuwa makini na wanyama pori wanaoingia kijijini humo. 

Mbunge Kamani yupo wilayani Busenda kwa mapumziko na kuendelea kuhamasisha shughuli mbalimbali za kimaendeleo katika jimbo lake.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA TAMU Published.. Blogger
Back To Top